Msanii G Nako
G Nako amefunguka hayo mbele ya kamera za eNewz ya EATV baada ya kuzua gumzo mtandaoni ikiwa ni siku chache tangu video hiyo ianze kuonekana na kuweka wazi hofu ya wazazi wake ingawa kwa asilimia kubwa ametimiza malengo yake.
"Wazazi wameogopa lakini, yani kuna hofu fulani ila tumewaelewesha na wameelewa. Nilichojaribu kukifanya ni sanaa tulijaribu kuwa creative na hakuna kingine ila asilimia nyingi wameelewa ila asilimia ndogo kidogo kama wameogopa na wamechukulia tofauti na jeneza lilikodishwa na watu wenye jeneza lao walikuwepo na baada ya kumaliza kulitumia walilichukua ili kwenda kulifanyaia kazi nyingine" G Nako alifunguka.
Aidha G Nako ameongeza kwamba "Vile watu waliposhtuka ndilo lengo letu lilipokuwa kwa maana ujumbe umefika. Pamoja na kwamba watu wameogopa wanatakiwa kukumbuka sote tutapitia hatua hiyo hivyo ukumbuke kufanya mema na kusali sana"
Picha ya G Nako ilozua tafrani mitandaoni