Jumamosi , 12th Aug , 2017

Malkia wa muziki wa Bongo fleva, Dayna Nyange, amesema akipata ujauzito, mashabiki wake wataamua njia gani aitumie kuwafahamisha.

Dayna, alisema kuanika nje tumbo wakati wa ujauzito ni jambo linalowezekana, lakini kwanza atawasikiliza mashabiki na baba mtoto wake.

“Kwa sasa hivi sijaamua kubeba ujauzito, lakini muda ukifika nitaweza kuachia wazi tumbo mashabiki wangu waone. Ninachoangalia nini mashabiki na baba mtoto wangu wanataka.” alisema Dayna.