Ijumaa , 13th Oct , 2017

Mwanamitindo Calisah ambaye hivi karibuni amekumbwa na skendo ya kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja baada ya kuonekana amevaa viatu vya kike, amesema anakusudia kufungua duka la kuwapa mimba wanawake.

Akizungumza kwenye eNewz ya East Africa Television, amesema anakusudia kufanya hivyo ili awasaidie wanawake wanaotaka kuzaa watoto wenye muonekano mzuri kama yeye, na wale ambao waume zao hawawezi kuzalisha kutokana na umri kuwa mkubwa (vibabu).

“Suala la kuzaa mimi mwenyewe ni kitu ambacho nilikuwa na plan nacho kwa sababu nimeshatoka na wanawake wengi, sema sikuwa tayari kuzaa mi bado kijana mdogo, hawa wote nilikuwa nao tu kwa mambo mengine, lakini kama kuna mtu atataka tuzae, naweka tu bao langu napiga inatoka pair flan kali, najua mtoto wangu atakuwa na maisha mazuri”, amesema Calisah.

Calisah ameendelea kwa kusema kwama...”Tunawajua wanawake wengi sana wazuri ambao wanaishi na wazee wana mapengo lakini ana hela, anajikuta anazaa naye kisa hela, tusijidharau wanaume, kwa hiyo mtu anakuja na mpunga wake nafanya chochote kwa pesa, mi kidume nanyoosha tu, aje tu na hela, kama wanawake wazuri wanatembea na watoto wazuri, kwa nini sisi wanaume tusifanye hivyo? Anakuja anatoa hela, tunapiga tunatoa pair yetu”.

Itazame vdeo yote hapa chini akizungumza hilo.