Ben Pol
Ben Pol amesema hayo kwenye kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio na kusema hata ikifika wakati wa kuoa ataoa kimya kimya kwani anaogopa asijekupoteza mashabiki zake kwenye muziki ambao huwa wanajipa moyo kupata nafasi hiyo.
"Mimi kuoa bado kidogo nafikiri itafika muda muafaka nitafunga ndoa, bado najipanga ila mimi naamini ndoa huwa ina tabia ya kuharibu career kidogo kwa asilimia kadhaa. Hivyo nitaoa kimya kimya kwa sababu sisi tuna mashabiki wengi na wengine wanaona huenda kukawa na nafasi kwao sasa ukioa wakajua unaweza kuwakosa hao kwenye muziki wako" alisema Ben Pol