Barnaba Classic
Akiongea kupitia eNewz ya EATV, Barnaba amesema "Naomba tena radhi kwa jamii kwa kauli ya Ice aliyosema kwamba mimi ndiye nimemchelewesha kufanikiwa katika muziki wake kwa kuwa sipendi kugombana na kukwanzana na mtu namuomba radhi kupitia eNewz kwamba anisameha kwa makosa yangu" alisema Barnaba
Hata hivyo Barnaba alisema siri ya mafanikio siyo kuvaa vizuri, kula vizuri au kuishi pazuri bali ni kuwa na heshima na kuepukana na malumbano na ugomvi usio wa lazima.
Mtazame hapa katika eNewz