Jumapili , 19th Feb , 2017

Msanii wa bongo movie Aunt Ezekiel amesema hana mpango wa kumuinginza mpenzi wake Mose Iyobo kwenye tasnia ya bongo movie. 

Aunt na Mose

Akionge kupitia eNewz Aunt amesema "Napenda anavyokuwa anacheza na sijawahi kuwaza kumtoa kwenye kipaji chake na kumuingiza kwenye movie  hata kama akitaka kuacha kipaji chake ni bora ajiingize kwenye biashara lakini siyo kujiingiza kwenye movie kwani siyo kipaji chake".

Hata hivyo Aunt amesema yeye hakuvutwa na mtu kuingia kwenye uigizaji na ndiyo maana alifanikiwa kupitia bongo v movie  hivyo yeye atabaki kuwa muigizaji na Iyobo atabaki na mauno yake.