Jumanne , 19th Sep , 2017

Msanii Baraka The Prince amesema yeye ni sawa na Rais Magufuli kwenye game ya bongo fleva, kwa kuwa na misimamo na itikadi ambazo wengi hawazipendi.

Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Baraka amesema misimamo yake na jinsi ambavyo hapendi kuona anaonewa, ndio sababu ya watu kutomkubali na ndio sababu ya kuhama hama kwenye uongozi.

Baraka amesema siku zote mtu ukiwa na mitizama na misimamo yako, lazima watu watakuona mbaya, huku akimtolea mfano Rais Magufuli jinsi alivyo na misimamo katika harakati zake za kutetea wanyonge, kitendo ambacho kinapingwa na baadhi ya watu wengi.

Msikilize hapa chii