Waziri Mwigulu Nchemba akiwa anafundisha
Waziri Nchemba ameshuhudia uwezo wa mwanafunzi huyo akiwa wakati alipoingia shuleni hapo na kuanza kufundisha somo la hesabu ambapo amefurahishwa na jinsi walimu wa shule hiyo walivyojitahidi kuweka juhudi zao katika kuhakikisha wanawasaidia watoto hao kutimiza malengo yao.
Waziri Nchemba akiwa kwenye ziara ndani ya jimbo la Iramba alipita shuleni hapo kusikiliza kero mbalimbali lakini pia kufuatilia hali ya taaluma ndani ya jimbo la Iramba ambapo ameshuhudia miundombinu mibovu inayohatarisha usalama kwa wanafunzi waliopo shuleni hapo na kuahidi kuirekebisha mapema iwezekanavyo.
Akiwa shuleni hapo Mh. Waziri ameahidi kujitolea kujenga nyumba za walimu pamoja na ukarabati wa vyumba vya madarasa ambavyo vinahatarisha usalama wa wanafunzi hao.
Waziri Mwigulu ametoa ahadi hiyo baada ya kutembelea shule hiyo na kusema mazingira wanayopitia waalimu pamoja na wanafunzi hao ni magumu sana ingawa walimu wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanafunzi hao wanafanya vizuri na kufikia ndoto zao.
Waziri Nchemba akimtazma mwanafunzi akikokotoa swali alilompatia
Waziri Nchemba ameshuhudia waalimu wanaokadiriwa kuwa tisa wa shule hiyo wakiishi pamoja katika nyumba chache zilizopo shuleni hapo huku vyumba vya madarasa navyo vikiwa si vyakuridhisha sana.
"Waalimu 9 kuishi kwenye nyumba tatu za aina hiyo siyo jambo la kuridhisha hata kidogo na pia siyo sahihi. Pamoja na changamoto mlizonazo niwapongeze sana kwani mnafanya kazi nzuri. Katika mazingira haya magumu lakini mnatoa watoto hapa wanaenda Mzumbe ni faraja kubwa. Nina uhakika miaka 15 ijayo humu watatoka wabunge wengi kwenye shule hii," Nchemba.
"Nawaahidi madarasa na nyumba za walimu kuwa nimechukua changamoto hizi na nitaleta 'cement' ya kiasi mnachohitaji mapema iwezekanavyo na nitakapofika mjini nitakutana na marafiki zangu pamoja na waziri ili tuweke mikakati ya kufanya marekebisho ya shule hii pamoja na hizo nyumba" Nchema aliongeza
Waziri Mwigulu ameshuhudia ubovu wa madarasa matatu ya shule hiyo yakiwa mabovu kabisa na yenye nyufa kubwa ambayo ni hatari sana kwa usalama wa wanafunzi huku madarasa hayo yakiwa hayana sakafu kabisa.
Msikilize hapa Chini