Alhamisi , 29th Oct , 2020

Zitto Zuberi Kabwe ambaye ni kiongozi muasisi na mwanadamizi katika Chama cha ACT Wazalendo, leo tarehe 29 Oktoba amekuwa miongoni mwa wapinzani nguli kwa ngazi ya ubunge kupoteza jimbo lake la Kigoma Mjini ambapo amepata kura 20,600 dhidi ya mshindi Kilumbe Ng'enda aliyepata kura 27,688.

Pichani ni aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Zitto Kabwe.

Kupitia ukurasa wake wa twitter ameandika '' Ngome nyingine ya upinzani imechukuliwa kwa mabavu, Jimbo langu limechukuliwa. Ni mapambazuko mpya.