Askofu wa makanisa ya Philadelphia Gospel Assembly, Dkt. Yohana Masinga.
Akizungumza na East Africa Television Askofu Mkuu wa Makanisa ya Philadelphia Gospel Assembly, lenye makao makuu yake jijini Dodoma Dkt. Yohana Masinga, amesema wagombea walioshindwa wasikate tamaa kwani wanatakiwa kujaribu kipindi kijacho.
Kwa upande wake Askofu wa kanisa la AGT Ipagala Dkt. Evance Chande, amesema kuwa wagombea walioshindwa ni kutokana na kile walichopanda kwa wananchi na hivyo amewaomba washirikiane na washindi.