Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro
Akizungumza Mkoani Kilimanjaro, ambapo sherehe za Idd zinatarajiwa kufanyika kitaifa ambapo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa atakua Mgeni Rasmi, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amesema jeshi hilo halitamvumilia mtu yoyote atakayefanya uhalifu katika msimu huu.
IGP Sirro amewataka waislam kuendeleza matendo mema waliyokuwa wakiyafanya katika kipindi chote cha Mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani ikiwemo kudumisha umoja, amani na ushirikiano.
Pamoja na hayo ameongeza kwamba, Sherehe hizo zinaunganisha taifa pamoja na dunia nzima kwa furaha na amani hivyo, Watanzania hawana budi kudumisha amani ya nchi iliyopo kwa sasa.