Roboti Omeife atakayezinduliwa leo
Mkurugenzi Mtendaji wa kikundi hicho, Chuks Ekwueme, ambaye alitangaza hayo katika taarifa yake jana mjini Abuja, alisema hafla hiyo itafanyika leo siku ya Ijumaa.
Ekwueme alisema roboti huyo wa kike wa Kiafrika mwenye urefu wa futi sita anazungumza lugha kama huduma kwa biashara zinazohitaji kuunganisha watazamaji asilia wa Kiafrika, akiongeza kuwa ni roboti ya kazi nyingi na msaada.
"Inawatambulisha wanadamu kupitia sura, ikizingatia kitu mahususi inapohitajika, inatambua vitu, inajua sifa zao na pia inakokotoa nafasi na umbali wa vitu inachokiona, inazingatia mtu maalum kuweka mazungumzo hai," amesema Mkurugenzi wa kampuni hiyo
Roboti hiyo inazungumza lugha ya Kiingereza, Kifaransa, Kiarabu, na pia lugha za Kiafrika, kama vile Kiswahili, Pidgin, Wazobia, Afrikaans na Igbo.
Jina Omeife ni la Kiigbo linalomaanisha "uwezo wa kufanya mambo mengi".