Jumamosi , 10th Dec , 2016

Kiongozi wa Gambia Yahya Jammeh amepinga matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika nchini humo mwezi huu wiki moja baada ya awali kuyakubali matokeo hayo.

Yahya Jammeh - Rais wa Gambia

 

Akiongea kupitia Television ya Taifa hilo Rais  Jammeh alidai kwamba kulikuwa na ukiukwaji mkubwa katika zoezi la kupiga kura na kutaka kuitishwa kwa uchaguzi mpya.

Jammeh ambaye aliingia madarakani kufuatia mapinduzi ya kijeshi mwaka 1994 alishindwa vibaya na mpinzani wake  Adama Barrow, ambaye alishinda kwa zaidi ya asilimia 45 ya kura zote.

Barrow ambaye ni mfanyabiashara anatarajiwa kuapishwa mwezi Januari mwakani.