Aliyekuwa mgombea ubunge Kenya Raila Odinga
Katika mkutano wake huo mtaa wa Kibera, jijini Nairobi, Bw. Raila amewaambia wafuasi wake wasiende kazini kesho akisema, Muungano huo utatangaza hatua watakayochukua Jumanne ijayo.
Kwa mujibu wa gazeti la The Star, kiongozi huyo pia anatarajiwa kuitembelea familia ya binti wa miaka kumi aliyeuwawa kwa kupigwa risasi wakati wa maandamano ya kupinga matokeo katika kitongoji cha Mathare, ambapo pia maandamano yalishuhudiwa maeneo ya Nyanza, Mathare na Kibera ambako watu wengine 10 wameuwawa.
Hata hivyo Kaimu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Kenya, Fred Matiang'i, amedai kutokuwa na taarifa za mtu yeyote kuuwawa kwa kupigwa risasi nchini humo, na kwamba huo ni uvumi
Kenya leo imeshuhudia utulivu baada ya vurugu hizo za Jumamosi, wakati Bw. Raila akikabiliwa na shinikizo kutoka Jumuiya ya Kimataifa kuyakubali matokeo ya uchaguzi.