Mganga mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Kagera, Dk. Mseleta Nyakiroto amekiri kupokea mwili wa mwanafunzi huyo wa kike na majeruhi mmoja wa kiume ambaye ni mwalimu katika shule hiyo, saa tano asubuhi.
Akizungumza akiwa hospitalini hapo majeruhi katika ajali hiyo ya radi Charles Alphonce ambaye ni mwalimu katika shule hiyo ya sekondari amesema kuwa wakati wa tukio alikuwa akitoa darasani kufundisha akiwa amefuatana na mwanafunzi huyo na kwamba ghafla aliona wingu kubwa la moto likishuka kuwafunika.