Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini SACP David Misime
Taarifa hiyo imetolewa na Msemaji wa Jeshi hilo, SACP David Misime, na kusema hadi sasa baadhi ya wahalifu wanaofanya vitendo hivyo wameshakamatwa na wengine bado wanaendelea kutafutwa.
"Huwatumia wanaowalenga kuwatapeli picha za mabanda ya maonesho, bidhaa au magari ili kuwaaminisha kuwa kuna maandalizi ya maonyesho yanaandaliwa na baada ya kufanya hivyo huwataka walipie ada ya ushiriki au walipe bidhaa hizo," amesema SACP Misime.