Masten Wanjala, Muuaji wa watoto zaidi ya 10
Msako mkali umeanza kumtafuta mtuhumiwa huyo baada ya polisi kubaini hayupo rumande wakati walipokuwa wanaitisha majina asubuhi.
Wanjala alikuwa anashikiliwa na polisi kwa uchunguzi wa mauaji ya mfululizo ya watoto yaliyolishtua taifa la Kenya.
Polisi waliokuwa zamu wakati mtuhumiwa huyo anatoroka kwenye kituo cha Jogoo Road eneo la Eastlands Jijini Nairobi wamekamatwa.