Jumatatu , 20th Nov , 2017

Mkurugenzi wa Mawasiliano,Itikadi na Mambo ya Nje     CHADEMA, John Mrema ametoa taarifa kwamba Mbunge wa Kibamba Mh. John Mnyika anatafutwa na Jeshi la polisi mkoani Songwe.

Taarifa aliyoitoa Ndg, Mrema haijaweka wazi sababu za kiongozi huyo kutafutwa na Jeshi la polisi ingawa taarifa hizo simekuja ikiwa ni siku moja kupita tangu Mnyika alipohutubia kwenye kampeni za uchaguzi.

"Mhe. John Mnyika, mara baada ya kuhutubia kata ya Ndalambo, wilayani Momba mkoani Songwe, jana Jumapili 19/11/2017, Jeshi la Polisi wilaya hiyo ya Momba linamtafuta. Tutaendelea kutoa taarifa kwa kadri zinavyotufikia," John Mrema