Alhamisi , 23rd Nov , 2017

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  Dkt. Vicent Mashinji amekanusha habari za kwamba anahamia Chama cha Mapinduzi na kusema kwamba yeye siyo mtu wa kuamini kwenye zidumu fikra za Mwenyekiti bali nguvu ya mamlaka ya umma.

Mashinji amesema kwamba yeye siyo mjamaa bali ni mlengo wa kipepari hivyo amewataka wananchi wawe na amani kuhusu hizo taarifa za yeye kuhamia CCM si za ukweli.

"Napokea simu nyingi eti nahamia CCM, mi si Mjamaa. Mi ni mlengo wa kibepari. Siamini kwenye “zidumu fikra za mwenyekiti” Ninaamini katika “nguvu na mamlaka ya umma”. Naomba ndugu zangu muwe na amani kabisa" Mashinji.

Dkt Mashinji ameongza kwamba "Nitaendelea kutumikia CHADEMA kwa makini na kutimiza ndoto za watanzania".