Mhe. Lema amesema hayo leo baada ya kuzungumzia suala la kamata kamata inayofanywa kwa amri ya wakuu wa wilaya na mikoa na kusema kwa jinsi jeshi la polisi linavyotumika siyo kila amri itakyotolewa itakuwa na maana ndani ya nchi kwani zigine zitalipeleka pabaya taifa la Tanzania.
"Hizi amri ambazo zinatolewa na kutekelezwa sizo nzuri. Mfano DC siku akisema Mbunge wa Arusha mjini apigwe risasi basi amri hiyo itatekelezwa nitapigwa. Kwa staili hii najua wapo watu ambao watakuja nyuma yetu au wengine ambao tupo nao sasa hivi watashindwa kuvumiliwa haya mateso na udhalilishwaji, ambao haipiti wiki mbinge wa upinzani anakuwa amekamatwa. Nakemea sana jambo hili," Lema alifunguka.
Pamoja na hayo Mhe. Lema amempongeza Rais Mteule wa Kenya, Mh. Uhuru Kenyatta kwa kuonyesha demokrasia ya kweli ya kuruhusu maandamano ya kuupinga ushindi wake huku akitoa na jeshi la kuwalinda raia katika maandamano hayo.