Alhamisi , 16th Feb , 2017

Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwan Kikwete amefunguka kuhusu madai ya baadhi ya watu kuwa ana utajiri wa kutisha na kwamba anamiliki mali nyingi, jambo ambalo limekuwa likifanya watu hao watilie shaka njia aliyotumia kupata utajiri huo.

Ridhiwan Kikwete - Mbunge wa Chalinze

Kikwete akiwa kwenye kipindi cha East Africa Breakfast ndani ya EA radio, amesema kuwa anashangazwa na dhana hiyo potofu inayojengwa na watu bila kujua ukweli wa mambo, ambapo ameweka wazi kuwa yeye ni kijana mpiganaji na mwenye kupenda mafanikio, lakini hana umiliki wa mali nyingi kama ambavyo imekuwa ikisemwa.

Ridhiwan ambaye ni mtotot wa Rais wa awamu ya nne wa Tanzania, Jakaya Kikwete, amesema mali zake ni za kawaida na amezipata kwa njia halali, huku akisimulia jinsi alivyowahi kuwakuta watu wakimjadili yeye kuhusu mali zake, bila watu hao kujua kuwa yeye ndiye Ridhiwan Kikwete.

Msikilize hapa akiwa katika mazungumzo na watangazaji wa kipindi, Irene Tillya, Shaaban Lupa na Songa wa Songa