Julius Mtatiro - Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF
Akizungmza leo na wanahabari jijini Dar es salaam Mtatiro amesema kuwa fedha hizo ni za Ruzuku ya chama, hivyo zimehamishwa Januari 5 mwaka huu,bila ya kuwepo kwa taarifa kwenye bodi ya udhamini wa chama hicho,nakuziomba mamlaka husika ikiwemo taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa Takukuru na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kufanya uchunguzi dhidi ya uhamishaji huo.
Kufuatia hatua hiyo CUF imeanza kuchukua hatua ikiwa ni pamoja na viongozi wa juu wa chama hicho,kuanza kukutana ili kujadili kile alichokiita kuwa ni shambulio ili kuchukua hatua za kisheria dhidi ya watu waliyohusika na utakatishaji na uhamishaji wa fedha hizo.