IGP Sirro amesema hayo akiwa katika Shule ya Polisi Tanzania, Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo amewataka wanafunzi hao kuzingatia mafunzo wanayoyapata na kuto kuchezea nafasi waliyoipata kwa kufanya vitendo vya utovu wa nidhamu na kupelekea kufukuzwa mafunzo hayo.
Shule ya Polisi Tanzania maarufu CCP inazaidi ya wanafunzi elfu nne wa kozi ya awali ya askari Polisi ambao wanapata mafunzo ya uaskari Polisi kwenye shule hiyo.