Jumatatu , 20th Nov , 2017

Chama cha Mapinduzi CCM kupitia Kamati kuu (CC) kwa niaba ya halmashauri kuu taifa NEC, kimefanya uteuzi wa wagombea walioomba kuwania nafasi ya Uenyekiti katika wilaya Sita nchini zikiwemo zile wilaya za kichama.

Wilaya ambazo zimepata wagombea ni Moshi Mjini, Siha na Hai zote za mkoani Kilimanjaro ambapo uchaguzi umepangwa kufanyika Desemba 1-2 mwaka huu. Wilaya ya Makete mkoani Njombe pamoja na wilaya zinazotambulika kichama za Musoma Mjini na Musoma Vijijini mkoani Mara uchaguzi wake umepangwa kufanyika Novemba 25-26 mwaka huu.

Katika Wilaya ya Hai walioteuliwa kugombea nafasi hizo ni Abdullah Hussein Mriri, Magai Wang’uba Maganda na Justice Edmen Elipokea Massawe. Wilaya ya Siha ni Justice Nicodemo Mkita, Wlfred Luka Mossi na Humfrey Joshua Nnko.

Wilaya ya Moshi Mjini ni Absalom Angyeulile Mwakyoma, Joseph Oforo Mtui, Faraji Kibaya Swai na Alhaj Omar Amin Shamba. Wilaya ya Makete ni Aida Menson Chengula, Mwamwite Clemence Njajilo na Onna Amos Nkwama.

Wilaya ya Kichama ya Musoma Mjini walioteuliwa ni Robert Maganya Sylvester, Magiri Benedicto Maregesi, Amina Marumbo Nyamgambwa na Daud Adam Misango. Wialya nyingne ya kichama ya Musoma vijijini wagombea ni Gerald Mfungo Kasonyi, Kananda Hamisi Kananda na Nyabukika Bwire Nyabukika.