Akizungumza na mwandishi wa habari wa East Africa Television mwenyekiti wa BAVICHA Muheza, Joseph Saja, amesema sababu ya zoezi hilo kutofanyika ni kwamba siku walizotangaza kuwataka waliofanya tukio hilo kujisalimisha zilikuwa hazijaisha, hivyo wataendelea na zoezi hilo mapema wiki ijayo.
"Siku ambazo tuliwapa wale watu kujitokeza ilikuwa mwisho Ijumaa, na mpaka leo bado hawajajitokeza sasa ndio tutatekeleza majukumu yetu ya kuanza kwenda huko tunakoenda kuisoma, inawezakana katika juma tatu au jumanne ndio tutatoka kwenda", amesema Joseph Saja.
Wiki iliyopita BAVICHA wilayani Muheza mkoani Tanga walitangaza kusoma albadili ili kuwajua watu waliomshambulia kwa risasi Tundu Lissu, na kuisaidia serikali ambayo mpaka sasa haijafahamu waliohusika.